Supa Nyamwela Afunguka Kuhusu ALI Choki Kuumwa..."Alikuwa Anaumwa Kwa Kipindi Kirefu"

Kiongozi wa chama cha wachezaji Tanzania, Supa Nyamwela amefunguka kusema  msanii wa bendi Ali Choki ni mzima wa afya japokuwa alikuwa anaumwa kwa kipindi kirefu.


Supa Nyamwela ameeleza hayo baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba Ali Choki amekimbia hapa  Dar Es Salaam na kukimbilia Jijini Mwanza kwa sababu ya matatizo yake ya kiafya.

"Ndugu yangu Ali Choki yupo kama kawaida bali ameamua kubadilisha upepo na maisha kwa kuishi jijini Mwanza,  naweza kukiri kwamba ni kweli alikuwa anaumwa kwa kipindi kirefu lakini sasa hivi mwili wake umerudi, yupo sawa, amerudisha afya yake, na anaendelea na kazi"  amesema Supa Nyamwela 

Aidha Supa Nyamwela ameongeza kusema  "Siwezi kusema alikuwa anaumwa nini ila Tanzania na Dunia ijue tu Ali Choki yupo sawa na amerudi kuliko yule wa zamani"

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad