Boris Johnson Awapongeza Madaktari kwa Kunusuru Maisha yake



Waziri mkuu wa Uingereza , Boris Johnson awapongeza madaktari  kwa kufanya kile kilichohitajika kunusuru maisha yake alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuambukiwa virusi vya corona.

Boris amewapongeza madaktari  kwa kile  alichojata kuwa wamenusuru maisha yake baada ya kulazwa hospitali  akiwa ameambukiwa virusi vya corona.

Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson ameruhusiwa kuondoka hospitali Jumapili  baada ya vipimo kuonesha kuwa hana maambukizi na kuwa afya yake ni salama.

Baada ya kuruhusiwa kuondoka katika  hospitali ya  Mtakatifu Thomas mjini London,  waziri mkuu  huyo ataendelea na  uchunguzi  akiwa nyumbani kwake  Chequers.

Boris hatorejea sasa hivi kutekeleza jukumu lake la waziri mkuu  hadi atakapothibitishiwa na madaktari kuwa na uwezo wa  kutekeleza majukumu yake.

Waziri  mkuu huyo  wa Uingereza amesema kwamba taifa lake limepiga hatua  katika  juhudi za kupambana na virusi vya corona.

Video iliopeperushwa katika ukurasa wake wa Twitter imemuonesha  Boris akiondoka hospitali  ambapo alikuwa akipatiwa matibabu yaliochukuwa muda wa wiki moja.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad