Breaking News: Wagonjwa wa Corona Tanzania Wafikia 284



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia katika tukio la ibada ya Kitaifa DSM leo Jumatano, amesema kufikia Jumanne Aprili 21 wagonjwa waliothibitika nchini humo ni 284 ambapo kati yao 256 wanaendelea vizuri, saba kwenye uangalizi maalumu, 11 wamepona na 10 wamefariki.

“Jumla ya wagonjwa 284 wamethibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona, kati ya hao wagonjwa 256 wanaendelea vizuri kiafya, wagonjwa 7 wako kwenye uangalizi wa karibu kadhalika wagonjwa 11 walishapona kabisa” Kassim Majaliwa,Waziri Mkuu wa Tanzania.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad