Madaktari 251 Wapata Maambukizi ya Virusi vya Corona


Takriban madaktari 251 nchini Bangladesh wamepata maambukizi ya Corona Virus, Taasisi ya Madaktari (BDF) imelalamikia ukosefu wa vifaa kinga (PPE) kuwa chanzo cha Madaktari kupata maambukizi kutoka kwa wagonjwa

Kufuatia ongezeko la waathirika wa COVID 19 nchini humo, Serikali imekuwa na changamoto ya kuwalinda watumishi wa afya ili wasipate maambukizi ya Virusi hivyo.

Bangladesh, kama ilivyo kwa mataifa mengi duniani inakabiliwa na uhaba mkubwa wa vifaa kinga kwa ajili ya watoa huduma za afya. Nchi hiyo imerekodi maambukizi 4,186 na vifo 127 hadi sasa huku waliopona wakiwa 108.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad