Museveni: Hakuna maambukizi ya ndani “visa vipya vinaletwa na Madereva wa Malori”



Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema hakuna maambukizi mapya ya ndani kwa siku nyingi Uganda na kusema huenda hiyo ina ashiria hakuna maambukizi tena ya corona au Watu wana virusi ila hawaugui , Museveni amesema  kwa mujibu wa Wataalamu wake kama Watu wana virusi na hawaugui ni jambo zuri kwakuwa wanapata kinga mwili na hata virusi vikiondoka vikarudi tena watapambana navyo.

“Bado tuna visa 79, wagonjwa wanapona kwa kasi hadi sasa wamepona 52 na hatuna kifo, visa vya ndani tumedhibiti kabisa, tuko vizuri, shida pekee kwa sasa ni visa vya nje vinavyoletwa na Madereva wa Malori, naambiwa Waganda wana hasira nao kweli, tusiwachukie jirani zetu”-MUSEVENI

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad