"Nataka Peter Msechu awe kama Vanessa" - Baba Levo


Diwani wa Mwanga Kaskazini Kigoma Ujiji na msanii wa BongoFleva Baba Levo, amesema huwa anamshambulia kwa maneno Peter Msechu kwa sababu anataka apungue hadi awe na mwili kama wa Vanessa Mdee.


Akizungungumza na EATV & EA Radio Digital, Baba Levo amesema huwa anajisikia raha pale anapomshambulia Peter Msechu na lengo lake ni kumtaka akonde na kumpa mawazo.

"Najisikia raha ninapomshambulia Peter Msechu, lengo la kumshambulia huwa nataka akonde na nimpe mawazo ili awe na mwili flani hivi kama Vanessa Mdee, nataka hata akitembea awe sawa na Vanessa, ila siwezi nikamtania hadi kumvunjia mipaka yake kwa mfano kufika hadi kwa wazazi" amesema Baba Levo

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad