Simba Yaingia 'Top 10', Klabu Maarufu Afrika


Klabu ya soka ya Simba imeingia kwenye nafasi 10 za juu katika listi ya klabu maarufu zaidi kwenye mitandao ya kijamii barani Afrika, ikishika namba nane kwa jumla ya wafuasi milioni 2.

Kwa mujibu wa mtandao wa Digital Sports Africa, wafuasi hao wametoka katika mitandao ya Instagram, Facebook, Twitter, YouTube, TikTok na linkedin, ambapo klabu ya Al Ahly ya nchini Misri inaongoza ikiwa na wafuasi milioni 27, ikifuatiwa na Zamalek SC yenye wafuasi milioni 12 na Raja Club Athletics ya Morocco ikishika nafasi ya tatu kwa wafuasi milioni 6.

Klabu ya Azam FC inakamata nafasi ya 13 katika listi hiyo ikiwa na wafuasi takribani wafuasi milioni 1 na klabu ya Yanga 957,000.

Hizi ni takwimu za klabu 20 bora katika mitandao ya kijamii barani Afrika.



Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad