Wananchi wa Tanga walia wizi wa koki za ndoo za maji tiririka



Na Rebeca Duce, Tanga.

Mkuu wa wilaya  ya Tanga, Tobias Mwilapwa ,amewataka  wananchi wa jiji la Tanga  kuacha tabia ya  kupuuzia  maagizo ya serikali juu ya mapambano didhi ya ugonjwa  wa homa ya mapafu inayosababishwa  na virusi vya Corana  aina ya Covid -19 ili kuepusha maambukizi  ya ugonjwa huo.

Mkuu huyo wa Wilaya  ameyasema hayo alipokuwa kwenye ziara yake ya muda mfupi ya kukagua maeneo ya standi ya daladala iliyopo Ngamiani na  zinazofanya safari zake wilayani Pangani  kwamba aweze kujione    jinsi ambavyo wananchi wanatekeleza maelekezo   yaliyotolewa na serikali ili kupunguza msongamano  wa watu na matumizi na vitakasa mikono.

Aidha alisema kwamba kwa hali ilivyo bado baadhi ya wananchi wanafanya mizaha juu ya tahadhari ya ugonjwa wa Corona kwani hawachukulii  kwa umakini badala yake wanapuuzia na kufanya utani wakiwa kama watu wasiohusika na maagizo ya serikali.

Sambamba na hayo baadhi ya wananchi wametoa malalamiko yao  juu ya uwizi wa koki za  ndoo za maji tiriri ambazo zilikuwepo maeneo ya standi ya Nagamiani kwa ajili matumizi ya wananchi wanaotumia usasfiri  wa magari hayo na kwamba hakuna namna nyingine ya kutumia maji tiririka.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao Bi Rukia  ambaye ni Mtendaji kata ya Ngamiani kati amesema  wananchi wamekosa majiji titirika baada ya koki zote kuibiwa na watu wasiowapendea mema wananchi wenzao kwani ndoo zote zimekutwa hazina koki na maji hayawezi kukaa tena kwenye hizo ndoo.

Akijibu malalamiko hayo mkuu wa wilaya Tanga Tobias Mwilapwa amewatahadharisha waliofanya uhalifu huo na kusema kwamba ni hujuma inayochelewesha mafanikio ya wananchi juu ya mapambano didhi ya maambukizi ya ugonjwa  Corona.

Alisema wapo wafanya biashara ambao wamepandisha bei za koki kutoka sh. 2500 hadi 7000 hivyo waache tabia hiyo na kuhurumia wananchi  wa hali ya chini ili waweze kuzinunua kwa ajili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Sambamba na hayo alisema kwamba wao kama serikali wakishirikiana  wanannchi wenye nia njema  tayari wamewabaini watu walioingia nchini kwa njia ya panya  wapatao 26 na kwamba kwa sasa wako karantini kwenye shule ya sekondari Usagara kwa ajili ya uchunguzi zaidi mapka  itakapofika siku 14 ya uangalizi ili hatua zingine zifutwe za kisheria.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad