Watoto Wachanga 8 Wakutwa na Virusi vya Corona Japan



Watoto wachanga wanane katika kituo kimoja cha malezi nchini Japan wamekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona baada ya mhudumu mmoja wa kituo hicho kupata maambukizi.

Hospitali kuu ya Saiseikai mjini Tokyo ambayo inakisimamia kituo hicho imesema watoto hao walioambukizwa wamelazwa hospitali wakati wengine 21 wamegundulika hawana virusi na wanaendelea kufuatiliwa.

Kituo hicho ni cha watoto yatima au watoto waliotenganishwa na wazazi wao kutokana na sababu za uwezekano wa kunyanyaswa au kutelekezwa.

 Bila ya kutowa maelezo mengi hospitali hiyo imetowa taarifa ikisema mhudumu wa kituo hicho alikutwa na maambukizi Aprili 16 na kusababisha kufanyika maamuzi ya kuwapima watoto wote
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad