Chadema Kwishney...Mbunge PETER Lijualikali Alia Machozi Bungeni na Kuomba Kuhamia CCM




Mbunge wa Kilombero (CHADEMA) Peter Lijualikali amemwaga machozi bungeni akidai kuadhibiwa na chama chake bila kusikilizwa. Amuomba Spika Ndugai kujiunga na CCM akisema yupo tayari kupewa kazi yoyote

Amesema "Nimefungwa miezi sita jela kwa sababu ya kukitetea chama changu, halafu leo eti wanasema nimerudi Bungeni kwa sababu ya posho. CHADEMA tumekuwa tukipigania uwepo wa Katiba ya nchi wakati Katiba yetu ya chama hatuifuati."

Ameongeza "Nilipohoji ndani ya chama changu kwamba baada ya kukaa karantini, tukirudi Bungeni tunarudi kwa hoja gani? Sikupewa majibu. Wabunge wa CHADEMA tunashindwa kumweleza Mwenyekiti kama anakosea. Hatuwezi kuwa wanademokrasia kama sisi hatuna Demokrasia"

Amesema "Kila mwezi Wabunge wa CHADEMA tunakatwa Tsh. Laki tano, eti kuchangia mfuko wa chama wakati wa kampeni, fedha zilipofika Tsh. Bilioni 8 na tulipohoji hizo fedha zipo wapi? Tukajibiwa uchaguzi ni chakato"
Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Nnavyo jua mimi, Chama kina UHAI.
    Hufika wakati kinakuwa Mahututi Bin Taabani, hapo kuna mawili kama HakiKufa basi Kinadhoofika sana, Sasa basi kwa Mbowe Kinaelekea HUKO.

    Poleni sana wenye Tai Shingoni.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mdau,hivyo kilikuwa Chama Genge?

      Uhuni na ubabaishaji ulitawala na KUJIMWABAFAI.

      Hivyomweenye Akili timamu anawezaje kuswagwa? Unapelekehwa tu hata hujitambui? kweli jameni

      Delete
    2. Mdau,hivyo kilikuwa Chama au Genge?

      Uhuni na ubabaishaji, Ulitawala na KUJIMWABAFAI.

      Hivyo mwenye Akili timamu, anawezaje kuswagwa? Unapelekeshwa tu, hata hujitambui? kweli jamani. Shtukeni.

      Delete
  2. Msajili wa Vyama vya Siasa.
    Athumani Diwani.
    Biswalo.

    Vyote mnakazi ya kufanya tena kwa Haraka.

    Na pia itapelekea kujua matukio tengenezi yanayo tumiwa na hili Genge au kikundi kilicho jificha katika ngao ya chama cha Siasa na pia kujua
    WANAMTUMIKIA NANI NA KWA MALENGO YAPI

    Lijualikali ni Mzalendo aliefunguka katika Bunge letu Sauti yetu Watanzania na kwa Uchungu wa Hhisia na
    Usalama wa nchiyetu aiweza kutoa chozi

    Pia kushindwa kwa Jitto kufanya nae kazi mpaka mkakati wa kutaka ku mmaliza kama ya aliyekuwa mbuge wa SGD Mashariki na kwenda kuanzisha chama cha Act.

    Kuna mengi yamejitokeza na majibu tunayataka . Cha zaidi ni hatua stahiki zichukuliwe ikiwemo 1 2 3 ..8

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad