Fahamu Kuhusu Historia ya Bibi Titi


Bibi Titi Mohammed alizaliwa Juni, 1926 na moja ya kumbukumbu tulinayo ya Mwanaharakati huyu katika Taifa letu ni Mtaa na Barabara ya Bibi Titi uliopo jijini Dar es salaam

Bibi Titi aliingia katika siasa kwa kushawishiwa na Schneider Plantan na yeye ndiye alikuwa muasisi wa Umoja wa wanawake Tanganyika (UWT) ulioundwa rasmi Mwaka 1963

Bibi Titi alikuwa na maneno makali dhidi ya ukoloni na alikuwa na ushawishi mkubwa. Akiwa na miaka 16 tu alikuwa mmoja kati ya wanawake wachache walioaminiwa katika kuongoza mapambano dhidi ya udhalimu waliokuwa wakifanyiwa Watanganyika

Baada ya Uhuru alichaguliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Ubunge, Uongozi wa Wilaya ya Rufiji na Mufindi, Rais wa Umoja wa wanawake Tanganyika(UWT) na baadae Waziri

Mwaka 1968 ,Bibi Titi pamoja na aliyekuwa Waziri wa ulinzi, Michael Kamaliza walikamatwa na kuhusishwa na matukio ya uhaini na wakahukumiwa kifungo cha maisha lakini mwaka 1972 waliachiwa kwa msamaha wa Rais

Alifariki Novemba, 2000 baada ya kusumbuliwa na matatizo ya moyo na kupelekwa katika hospitali ya Net Care, Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad