Hotuba ya Upinzani Yakataliwa KUSOMWA Bungeni, Spika Atoa Sababu


Hotuba ya Upinzani Yakataliwa KUSOMWA Bungeni, Spika Atoa Sababu

Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, ameikataa Hotuba ya Wizara ya Fedha kutoka Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, kwa kile alichokidai kuwa hotuba hiyo imeandaliwa na Mbunge ambaye hayupo ndani ya Bunge hilo.
Kupitia vikao vya Bunge ambavyo ameviendesha leo Mei 15, 2020, Bungeni jijini Dodoma Spika Ndugai ameendelea kusema kuwa, hajaikubali hotuba hiyo kwa kuwa mwandishi wa hotuba hiyo ni Mbunge Halima Mdee na hayupo ndani ya Bunge.
"Hotuba ya kambi rasmi hatujaikubali sababu mwandishi wake ni Halima Mdee ni kati ya wale waliojifukuza wenyewe Bungeni, kwamba roho zao ni muhimu kuliko wengine, haiwezekani ukapitishia dirishani kazi zako zikafanyika, wakati wewe hata uliko hakujulikani" amesema Spika Ndugai
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad