Profesa Kutoka China Aliyekuwa Akitafiti Corona Auwawa Marekani


Mauaji ya raia wa China, mtafiti wa masuala ya virusi vya corona kwenye ardhi ya Marekani yamesababisha nadharia mbalimbali duaniani kuwa kuna sababu iliyojificha kuhusu kifo chake.

Bing Liu, profesa msaidizi mwenye miaka 37 katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Pittsburgh, Marekani alipatikana akiwa amekufa nyumbani kwake siku ya Jumamosi.

Wenzake walisema alikuwa karibu kupata "matokeo muhimu" ya tafiti kuhusu Covid-19, tukio lililosababisha kuwepo kwa maoni mitandaoni yanayoeleza kuwa yawezekana bwana Liu aliuawa lakini polisi wanasema ni tukio la kujiua.

Alikutwa akiwa na majeraha mengi ya risasi kichwani,shingoni katika eneo la Pittsburgh yalipo makazi yake kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo.

Mtu aliyekuwa na silaha alitambulika kuwa na miaka 46, mhandisi wa programu ya kompyuta, Hao Gu. Mamlaka zinasema muuaji naye alijiua baada ya kurudi kwenye gari lake.

Liu na Gu walikuwa wanafahamiana, maafisa wapelelezi wa mauaji walieleza.

Uchunguzi umebaini kuwa lilikuwa tukio la kuua na kujiua lililotokana na ''mgogoro wa muda mrefu wa masuala ya kimapenzi''.

Wamesema ''hakuna ushahidi'' wa kuhusisha tukio hilo na utafiti wa Liu na mazingira ya sasa ya changamoto za kiafya.

Katika taarifa yao , wenzake wamemwelezea kama mtafiti wa kipekee ambaye ''alikuwa ukingoni kufanikisha kupata matokeo muhimu '' ya kuelewa maambukizi ya Covid-19.

Waliomboleza kifo cha Liu na kuahidi kumalizia utafiti wake ''zikiwa ni juhudi za kuenzi ubora wake katika uwanja wa kisanyansi''.

Liu, raia wa China alipata shahada yake ya kwanza na shahada ya uzamivu katika masomo ya sayansi ya kompyuta nchini Singapore kabla ya kufanya utafiti nchini Marekani.

Aliwahi kuungana na wanabaiolojia wengine kufanya utafiti kuhusu kinga ya binaadamu, kwa mujibu wa wasifu wake mtandaoni.C

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad