Wafanyabiashara wa Mafuta Wanaoficha Nishati Hiyo Kukiona




Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Innocent Bashungwa amesema kuwa serikali itawachukulia hatua wafanyabiashara wote wa mafuta walioficha nishati hiyo na kuacha kuuza kulingana na bei elekezi.

Waziri Bashungwa ametoa onyo hilo wakati wa kikao cha pamoja na mamlaka zinazosimamia kodi (TRA) , Nishati (EWURA) na Tume ya Ushindani (FCC) kujadili sababu na hatua zitakazochukuliwa kwa wafanyabiashara watakaobainika kwenda kinyume na sheria.

Amesema kutokana na janga la Covid-19 bei ya mafuta katika soko la dunia imeshuka huku ikichangiwa zaidi na mkakati uliowekwa wa ununuaji wa mafuta kwa pamoja, ambapo pia ametaja sheria zitakazotumika kuwakamata wanaoficha mafuta.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad