ADAM MCHOMVU amuaomba msamaha MBASHA baada ya kumpiga mtama jukwaani, Aandika haya



Ameandika Adam Katika Ukurasa wake wa Instagam:

"Dear #WashkajiZangu
kwanza nimuombe radhi Rais wetu wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Pili kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuniamini na kunipa nafasi ambayo bahati mbaya ilitokea tukapishana kauli jukwaani na bwana ndugu Msanii mwenzangu. Nimepokea simu mbalimbali za Viongozi wa Serikali wakinifahamisha namna nilipaswa kufanya wakati wa shambulio lile la mimi kuitwa 'ADAM Unajua we ni Bangi sana' Kwa pamoja nimewaelewa.
.
.
Nikutake radhi pia Emmanuel Mbasha Mimi sina tatizo lolote binafsi na Wewe kilichotokea ni kukwazika na kauli yako uliyotoa dhidi yangu kwenye tukio kubwa la Kitaifa lililotazamwa na Mamilion ya Watanzania. Sisi wote Vijana kuna muda tunakosea na tunawekana sawa japo njia zingine si nzuri. Asante kwa Jeshi la Polisi chini ya IGP Simon Sirro kwa maelekezo yenu. Nitayatii na kwa sasa mimi ni Balozi wenu wa hiari kabisa.." Adam

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad