Arsenal yaichapa MK Dons mechi ya kirafiki




Kiungo Mmisri, Mohamed Elneny akiifungia Arsenal bao la kwanza dakika ya tano katika ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji, Milton Keynes Dons FC kwenye mchezo wa kirafiki Uwanja wa MK (Milton Keynes), Buckinghamshire. 


Mabao mengine ya Arsenal yamefungwa na Eddie Nketiah dakika ya 10, Mark McGuinness dakika ya 76 na Reiss Nelson kwa penalti dakika ya 85, wakati bao pekee la MK Dons lilifungwa na  Rob Holding aliyejifunga dakika ya 32 na sasa kikosi cha Mikel Arteta kitaivaa Liverpool Jumamosi katika mechi ya Ngao ya Jamii.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad