Aslay azushiwa kifo, aitaka TCRA kuchukua hatua



Nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Aslay  ameeleza kusikitishwa na taarifa za yeye kuzushiwa kifo.

Aslay kupitia ukurasa wake wa #Instagram, ameomba mamlaka zinazohusika kufuatilia kiundani suala hilo. Chini ni kile alichoandika.


"Inasikitisha na kushangaza sana unawezaje kumzushia mwanadamu mwenzako kifo na mabaya mengi. Wanaofanya hivi ni Watanzania wa kawaida kama sisi ambao tulitamani watupe habari na burudani na wao wapate riziki, lakini wako bize kutupotosha na hata kuharibu majina yetu.


Nawaomba sana TCRA wasiache kuzichukulia hatua online Tv kama hao #GeeMedia #Mautamu na makanjanja wengine wanaopotosha umma. Tuna imani na ninyi TCRA, Jeshi la Polisi na mamlaka nyingine.


Watu kama hawa wakiachwa, wanachafua taswira nzuri ya vyombo vingine vinavyofanya kazi kwa weledi. Mimi naheshimu sana waandishi wote bila kujali ukubwa wa vyombo vyao, lakini hawa makanjanja wachukuliwe hatua na kutokomezwa kabisa".

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad