Babu Tale Amfungukia Marehemu Mke Wake Baada ya Kupita Bila Kupingwa Nafasi ya Ubunge Morogoro
0Udaku SpecialAugust 25, 2020
“Ni miaka minne tangu tumepiga hii picha, na ndio siku ambayo tulipoanza kupanga mikakati ya kwenda kugombea Ubunge katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki kwa lengo la kuendelea kutoa mchango wetu katika Jamii” - Hamisi Taletale maarufu kama @babutale
“Leo mwenzangu haupo ila najua uko ulipo unaona Mumeo nimeshinda/nimepita bila kupingwa nikimaanisha kuanzia leo mimi ni Mbunge wa Bunge la JMT anayesubiri kuapishwa tu na nipo tayari kwenda kumsaidia Mgombea Urais CCM Mzee wangu Magufuli kujaza kura zake nyingi za NDIO” -BABU TALE
“Mke wangu nitakukumbuka sana Mke wangu, nitayaenzi yote tuliyokubaliana kufanya, nitakuwa Mbunge Mtumishi wa watu wote na sitoacha kuisimamia taasisi yako ya ‘NASIMAMA NAO’, Nakupenda mke wangu ningefurahi tungelikuwa wote kusherehekea ndoto yetu, upumzike kwa Amani” -BABU TALE