Breaking News:Nyalandu ashinda kura za maoni Ubunge jimbo la Singida Kaskazini



Aliyewahi kuwa Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu, ambaye Oktoba 30 mwaka 2017 alitangaza kujiuzulu ubunge na kuhamia Chama Cha Demnokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo mapema alitangaza nia yake ya kurejea kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubunge wa jimbo hilohilo alilolitumikia kwa miaka 17 tangu mwaka 200-2017.


Baada ya ujumbe huo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ameandika kuwa ameshinda kura za maoni na atagombea Ubunge kwa mwaka 2020.


''Matokeo ya kura za maoni Singida Kaskazini, Kura zilizopigwa 229, kura halali 228, kura iliyoharibika 1, David Jumbe amepata kura 31 (13.53%) na Lazaro Nyalandu amepata kura 197 (86.02%)''

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad