Jamaa Aliyetabiri kifo chake mwezi Agosti 2019 amefariki dunia Agosti 2020




Jamaa mmoja kutoka kaunti ya Meru aliyetabiri kifo chake mwezi Agosti 2019 amefariki dunia Agosti 2020

Kupitia mtandao wa Facebook Abdulmalik Juma Baitairi alikuwa ameposti kuwa mwezi wa Agosti huwa muhimu kwa maisha yake kwani matukio mengi hutendeka mwezi huo.

Jamaa aliyetabiri kifo chake Agosti 2019, afariki mwaka mmoja baadaye

Jamaa aliyetabiri kifo chake Agosti 2019, afariki mwaka mmoja baadaye

Baitairi alikuwa amesema huenda angefariki dunia mwezi Agosti na kwa kweli utabiri wake umetimia.


" Mwezi Agosti huwa muhimu sana kwangu, nilizaliwa Agosti, ni mwezi huu ambao pia nilipashwa tohara, pia nilijiunga na chuo kikuu mwezi huu, ni mwezi ambao huenda nitaaga dunia, nani ajuaye?, Sherehekea mwezi huu wa mfalme," Aliandika Baitari.



Haijabainika kilichosababisha kifo chake lakini taarifa za karibu ziliarifu kuwa alikuwa akiugua ugonjwa wa kongosho na alikuwa akipokea matibabu Nairobi Hospital.


Mashabiki wake mitandaoni wameomboleza kifo chake kwa kutuma salamu za pole kwa marafiki na familia.

Marehemu amemuacha mjane na watoto wawili.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad