Kwanini Watu Maarufu Wengi ni Andunje?


Kautafiti kadogo nilikofanya chinichini kanaonyesha kuwa watu wengi maarufu hapa nchini ni "pipiro" aka andunje... yaani ni wafupi wa kimo.

Ukianzia kwa wasanii wetu wa muziki, bongofleva, maigizo, bongo muvi nk wengi ni vifupi balaa.. sitaki kutaja majina lakini kwa mnaowafahamu mtatupa uthibitisho. Na hii ni kwa wote wakiume na wakike.

Hata watangazaji wengi wa radio, tv nk yaani ukikutana nae "live" huwezi amini kama sauti ni yakwake kwa jinsi kalivyo kafupi.

Hata ukija mitandaoni ma slay queen wengi hasa wale wenye shape za maana na "ngongingo" kinachowaangusha ni wafupi hatari..

Je, kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya ufupi na umaarufu?

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad