Mbunge wa CUF Awapongeza CCM


Mbunge wa Tanga kupitia Chama cha CUF aliyemaliza muda wake, Mussa Mbarouk, amekipongeza Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanya maamuzi sahihi ya kutokuwarudisha wagombea waliotoka CUF na kutimkia CCM na kuacha Udiwani katikati kabla ya muda wao kuisha.



Kauli hiyo ameitoa wakati wa mahojiano na EATV na kusisitiza kuwa kwa dhati ya moyo wake, anakipongeze Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa kuhakikisha watu hao hawarudi kwani hii itakuwa fundisho kubwa kwa watu wenye tabia za kuhamahama.



"Wanaosema CUF imekufa ni wale waliokuwa na nia ovu na chama chetu, sasa wametoka na kuhamia vyama vingine, wale walioenda CCM mnajua kilichowatokea maana wenye chao hawakukubali kukaribisha wageni kwa sababu wapo waliokipatia tabu chama chao,  mimi nawapongeza CCM kwa kuwapiga chini wale Madiwani waliotoka CUF na kuhamia CCM", amesema Mbarouk.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad