Raia wa nchi 130 kuingia Kenya bila Karantini


Mamlaka nchini Kenya zimetoa orodha mpya ya raia wa nchi 130 ambao wataruhusiwa kuingia nchini humo bila kukaa karantini.



Hata hivyo, Taifa jirani la Tanzania halimo katika orodha hiyo. Kwa nchi za Afrika Mashariki ni Rwanda na Uganda ndizo zilizomo kwenye orodha hiyo.



Kenya ilifungua anga lake Agosti Mosi na Tanzania pia haikuwemo kwenye orodha ya awali. Hali hiyo ilisababisha mamlaka za Tanzania kuzuia ndege za Shirika la Ndege la Kenya kutua nchini humo.

Licha ya viongozi wa pande zote mbili kusema wanafanya mazungumzo, bado undani ama matokeo ya mazungumzo hayo havijawekwa wazi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad