Application ya TikTok inayomilikiwa na kampuni ya Kichina ya ByteDance imefungua mashtaka dhidi ya Serikali ya Marekani kupinga jitihada za utawala wa Rais Donald Trump kuzuia kampuni hiyo kufanya kazi Marekani
Wamesema hawachukulii suala la kuifungulia mashtaka Serikali kwa wepesi, lakini wanaona hakuna njia nyingine zaidi ya kufanya hivyo ili kulinda haki zao, na zile za jamii na wafanyakazi wake
Aidha, TikTok imesema zuio la Marekani limepuuza jitihada za kampuni hiyo kuthibitisha kuwa haitoi taarifa za wateja kwa Serikali ya #China, na kwamba sio kitisho kwa Usalama wa Taifa