Watu 13 Wauawa Katika Harakati za Kusisitiza Lockdown'



Watu 13 wameripotiwa kufariki na wengine watatu kujeruhiwa nchini Peru. Watu hao walionekana kukiuka sheria ya kubaki ndani na Polisi walitaka kuwakamata

Watu zaidi ya 120 walikuwa katika kusherehekea kwenye Klabu moja kinyume cha sheria. Peru imeweka suala la kuwekeana umbali kati ya mtu kuwa lazima na pia wamezuia kabisa mikusanyiko ya watu

Wizara ya Ndani imesema Polisi hawakuwa na silaha za moto bali watu hao walifariki wakiwa wanakimbia kuwaepuka Polisi. Uchunguzi wa kumjua mmiliki wa Klabu hiyo unaendelea huku watu 23 wakiwa wamekamatwa

Peru ni kati ya nchi za kwanza kuchukua hatua dhidi ya #COVID19 lakini ni taifa lililoathirika zaidi kwa mataifa ya Latin America, ikiwa na maambukizi 576,000 na vifo 27,000 vya #COVID19

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad