Ang’atwa na Nyoka Akichat na Simu Chooni



Kijana Siraphop Masukarat mwenye umri wa miaka 18 kutoka Thailand amejikuta katika hali mbaya baada ya kuumwa sehemu zake za siri na nyoka akiwa msalani.

Siraphop Masukarat alikuwa ameketi msalani/chooni huku akitazama video kwenye simu yake Jumanne, Septemba 8,2020 wakati alipohisi uchungu katika nyeti zake na kukimbizwa hospitalini ambapo madaktari walipendekeza ashonwe katika nyeti zake.

Akizingumza na Daily Mail, Siraphot alisema aligundua ameumwa na nyoka huyo baada ya kumuona akiinua kichwa chake.

“Nilikuwa najisaidia wakati ghafla nilianza kuhisi uchungu kwenye nyeti zangu. Ghafla nilimuona nyoka akiinua kichwa chake. Nilianza kutokwa na damu” Siraphot

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad