Kilichowaachanisha Rado na Irene Uwoya


Kupitia EATV & EA Radio Digital msanii wa filamu Rado ametusanua kwamba aliwahi kuwa kwenye mahusiano na msanii mwenziye wa filamu Irene Uwoya ila hakuwahi kutangaza kuhusiana na hilo.


Rado amesema mahusiano yao yalidumu kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia 2012 hadi 2013, na chanzo cha kuvunjika kwa penzi lao ni kupishana kwa maono na mitazamo tofauti.

"Mimi sio mtu wa kusemasema eti nikiwa na mahusiano na mtu fulani nianze kutangaza, mimi kuwa na Irene Uwoya sio stori ni vitu ambavyo vilitokea kwenye maisha yangu, sababu ya kuachana kwetu ni kuwa na maono tofauti na tukaona hatuwezi kwenda pamoja hivyo tukaachana kwa amani ila tumebaki kuwa washkaji" amesema Rado

Aidha msanii huyo amemsifia mpenzi wake wa zamani kwa kusema kwenye tasnia ya filamu Bongo hakuna mwanamke kama Irene Uwoya pia ni mzuri na mwanaume yeyote lazima atamani kuwa naye.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad