Magufuli Apiga Simu ‘Laivu’ Kwa Waziri Jafo, Ampa Maagizo



Mgombea Urais kupitia (CCM) Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho tawala na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa anaongea na wananchi wa Kazuramimba wilayani Uvinza mkoani Kigoma wakati akiwa njiani kuelekea Urambo mkoani Tabora tayari kwa mikutano yake wa kampeni leo Jumapili Septemba 20, 2020.

MGOMBEA Urais Kupitia tiketi ya CCM, Dkt John Pombe Magufuli, leo Septemba 20, 2020 ameendelea na kampeni zake za kituo kwa kituo akiwa safarini kutoka Kigoma Kuelekea Tabora.

Akiwa Uvinza aliposimama kuzungumza na wananchi, Magufuli amempigia simu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Selemani Jafo na kumtaka apeleke pesa bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Uvinza yenye urefu wa KM 10.Magufuli Apiga Simu ‘Laivu’ Kwa Waziri Jafo, Ampa Maagizo

Picha mbalimbali zikionesha Baadhi ya wananchi wa Kazuramimba wilayani Uvinza  mkoani Kigoma waliojitokeza kumlaki Mgombea Urais kupitia  (CCM) Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho tawala na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiwa njiani kuelekea Urambo mkoani Tabora.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad