Lil Wayne azua tafrani mtandaoni



Rapa kutoka nchini Marekani Lil Wayne amezua tafrani mtandaoni baada ya kutangaza kuwa amekutana na rais wa Marekani Donald Trump huku akiafikiana na mpango wa Rais huyo unao fahamika Kama "Platinum Plan" unao lenga kuwasaidia wamarekani wenye asili ya Afrika.

“Nilikuwa na kikao na Trump ukiachana na yale aliyofanya mpaka sasa mpango wake “The plutnum plan” unakwenda kuipa jamii umiliki halali.


Amesikiliza tulichotaka kusema na ametuhakikishia atatekeleza.”


Mapokeo ya wafuasi wake hasa nchini Marekani yalikua ni ya kumzomea na kumcheka huku wengine wakimtengenezea vibonzo vya kumdhihaki.


Pia wapo ambao walihisi ukurasa wake wa twitter umedukuliwa.


Hata hivyo baadhi ya wafuasi wa Trump wamefurahishwa huku wakiamini ni fursa hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa Marekani.


Rapa wengine wenye asili ya Afrika walio wahi kumuunga mkono trump ni Kanye West ambaye baadae alibadili mawazo na kuamua kusimama kama mgombea urais nchini Marekani.


Mwingine ni 50 Cent ambaye pia alibadili mawazo akisema “Sijawahi kumpenda”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad