Uwanja wa Ndege wa Bujumbura wafunguliwa Burundi



Kuanzia siku ya Jumapili, Uwanja wa ndege wa Bujumbura umefunguliwa kwa ajili ya ndege zinazofanya safari kimataifa baada ya kufungwa kwa miezi saba kutokana na janga la virusi vya corona.

Burundi imekuwa nchi ya mwisho ya Afrika mashariki kufungua anga yake baada ya Tanzania mwezi May, Sudani Kusini mwezi Julai, Kenya na Rwanda mwezi Agosti na Uganda mwezi Septemba.


Mamlaka ya anga imesema, abiria watakaoingia watahitajika kuwasilisha cheti kinachoonesha majibu ya vipimo vilivyofanywa saa 72 zilizopita yanayoonesha kutokuwa na maambukizi ya virusi, kufanyiwa vipimo na kukaa karantini kwa saa 72, kwa gharama zao.


Melance Ndayisenga, mkazi wa jiji la Bujumbura, amefurahishwa na kufunguliwa kwa uwanja wa ndege lakini amesema sekta ya utalii imeporomoka kutokana na kufungwa kwa uwanja huo wa ndege.


Burundi mpaka sasa imerekodi maambukizi kwa watu 421 na kifo cha mtu mmoja.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad