Vijana wa Nigeria watishia kufanya maandamano mapya



Ripoti za kuwepo kwa maandamano mapya nchini Nigeria zimechapishwa na vyombo vya habari vya nchini humo.

Vitisho hivyo vya maandamano mapya dhidi ya ukatili wa polisi vimejitokeza baada ya mahakama kutoa amri kuipa haki mamlaka Benki Kuu ya Nigeria kuzuia akaunti za watu 19 na kampuni zilizohusishwa na maandamano ya #EndSARS.


Makundi tofauti, ikiwemo ya haki ya kiislamu (Muric), wamewataka watu wasishiriki kwenye maandamano mapya.


Serikali ya Lagos pia imetahadharisha wakazi wake kutoshiriki maandamano.


Jopo liliundwa kuchunguza matukio ya ukatili wa polisi limekuwa likiwasikiliza waathirika.


Polisi imetoa tahadhari kuwa hairuhusu maandamano nchini humo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad