Nigeria: Boko Haram wawaua wanavijiji mkesha wa Krismasi





Watu kadhaa wameuawa kaskazini mashariki mwa Nigeria baada ya wanamgambo wa Boko Haram kushambulia vijiji vya Wakristo na kuteketeza Kanisa mkesha wa Krismasi.
Wapiganaji waliingia Pemi katika jimbo la Borno, kwa kutumia magari na piki piki na kuanza kufyatua risasi kiholela, mmoja wa viongozi katika kijiji hicho aliambia shirika hilo la habari.

Pemi iko karibu na Chibok ambako wasichana 200 wa shule walitekwa mwaka 2014.

Boko Haram wamefanya mashambulio kadhaa kaskazini mwa Nigeria ambako wanapigana kupindua serikali ili kubuni taifa la Kiislamu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad