Jaribio la Kusaidia ndoa ya Kim Kardashian na Kanye West Limegonga Mwamba.

 


Taarifa toka mtandao wa PEOPLE zinaripoti kwamba wawili hao walikuwa kwenye baraza la ushauri wa masuala ya ndoa lakini wameamua kuacha kuhudhuria kabisa na ni dalili kwamba Talaka inanukia.


Mbali na kusikia upande mmoja tu kwamba Kim Kardashian amekuwa akizungumza na mwanasheria wa masuala ya talaka, Kanye ameripotiwa kufanya hivyo pia.


Hata hivyo sababu za wawili hao kuachana zinaelezwa kuwa ni kukua kiakili kwa Kim Kardashian, kuwa serious na masomo yake ya Sheria, harakati na kampeni zake za kutetea wafungwa, huku wakati huo huo Kanye yeye akizungumzia masuala ya kugombea Urais na mambo mengine ya kipuuzi. Hivyo Kim anaelezwa kuchoshwa!

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad