Katibu Mkuu Wizara ya Afya " Tatizo Katika Mfumo wa Kupumua Sio Kuumwa Corona tu"


Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Mabula Mchembe amesema kuwa na tatizo katika mfumo wa kupumua sio kuumwa #CoronaVirus, hivyo watu wasiogope kwenda Hospitali


Ameeleza hayo baada ya ziara yake Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Bugando na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure, ikiwa ni mwendelezo wa kukagua hali ya utoaji Huduma za #Afya Nchini


Amefafanua, sio kila wagonjwa ambao wanahitaji Huduma ya Mfumo wa Hewa wanahitaji kupewa utambuzi (diagnosis) kuwa na Corona, kwani kuna wenye matatizo mengine ikiwemo Kisukari na Presha


Aidha, ametoa wito kwa Wananchi kujenga tabia ya kupima Afya mapema ili kutambua hali zao na kupata matibabu bila ya kuchelewa, kabla ya kupata matokeo ya hali ya kushindwa kupumua


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad