Magufuli Asema Wapo Wanaopenda Kunyongwa



Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema licha ya kutoa msamaha kwa wafungwa 265 waliokuwa wakisubiri kunyongwa siku chache zilizopita, bado kuna wafungwa wanatamani kunyongwa katika gereza kuu Isanga mjini Dodoma.


“Kwa hiyo watu wapenda kunyongwa, nimesamehe 265 nikasema jamani mkono wangu huu nisinyonge lakini leo nimeenda Isanga nimekuta 78 wanasubiri niwanyonge kwa sababu wamefanya makosa hivi karibuni,” amesema Rais Magufuli.



Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Februari 4,2021 wakati akiweka jiwe la msingi katika kiwanda cha samani cha Jeshi la Magereza ikiwa ni saa chache baada ya kuzindua ujenzi wa nyumba 20 kati 213 za maofisa wa gereza kuu la Isanga mjini Dodoma.

 DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL HAPA KUPATA HIZI HABARI KWENYE SIMU YAKO HATA BILA BUNDLE


“Unaweza kujiuliza saa zingine uongozi ni msalaba na nimeona maeneo ya kunyongea mpaka nimeogopa. Hata aliyekuwa ananieleza nilikuwa nashangaa tu hivi hajanyonga kweli huyu mbona maelezo yanaenda vizuri sana l
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad