RC Chalamila: Marufuku kutumia neno kifo cha ghafla



Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema kumekuwa na tabia iliyojitokeza siku za hivi karibuni kwa wakazi wa Mkoa huo kutoa taarifa katika mitandao ya kijamii ya kifo cha mtu kuwa amekufa ghafla, amesema kuanzia leo hataki kusikia taarifa hizo.

Chalamila ameyasema hayo akiwa Wilayani Kyela katika maadimisho ya Miaka 44 ya kuanzishwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Chalamila amefikia kutoa kauli hiyo baada ya kuona taarifa za namna hiyo zimekuwa zikiongezeka na kupelekea kuleta taharuki katika Mkoa wake, kitu ambacho kitapelekea wageni kutoingia mkoani hapo na kupelekea kukosekana kwa mapato.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Chalamila, wewe kweli ni kiboko, unaona mbali kama Ole Sabaya na Ali Hapi.
    Kunenge nae anajaribu. Hongera sana. Chapeni Kazi.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad