Rwandair yasitisha safari zake za Afrika Kusini




Kampuni ya ndege ya Rwanda, Rwandair imesitisha kwa muda safari zake katika mataifa ya Afrika Kusini, Zimbabwe na Zambia.
Kampuni hiyo imesema imechukua uamuzi huo kutokana na aina mpya ya Covid-19 inayoripotiwa katika mataifa ya kusini mwa Afrika.

Safari zote za kutoka na kuelekea katika miji ya Johannesburg, Cape Town, Lusaka na Harare zimesitishwa mara moja kuanzia Jumatatu.

Kampuni hiyo ya ndege imewatolea wito wateja wake waombe kurudishiwa fedha na kupanga upya safari zao.

Taarifa kamili ya kuahirishwa kwa safari za Rwandair ilitumwa kwenye mtandao wa kijamii wa twitter:

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad