Upinzani wakataa kumtambua Farmajo kama Rais wa Somalia





Viongozi wa upinzani nchini Somalia wamesema kuwa hawamtambui tena Rais wa nchi hiyo baada ya siku ya ukomo ya uchaguzi kupita na muda wa kuwa madarakani wa Mohamed Abdullahi Farmajo kumalizika.
Mazungumzo kati yao na serikali kuu ya jinsi ya kusonga mbele na uchaguzi huo yaligonga mwamba Ijumaa iliyopita.

Wanasiasa wa upinzani wametoa wito wa kuundwa kwa jopo litakalosimamia mamlaka ya mpito.

Kuna hofu kuwa mgogoro huo huenda ukasababisha kundi la wanamgambo la Al Shabab kuhangaisha raia.

Mgogoro wa kisiasa na ukosefu wa utawala ni hatari zaidi kwa taifa la Somalia ambalo tayari lipo katika hali tete.

Huku muda wa utawala wa Rais Framajo ukiwa umemaliza rasmi, viongozi wa upinzani wametoa wito kwa jeshi la taifa kuacha kuchukua maagizo kutoka kwake.

Ikiwa mambo yangeenda kama ilivyokuwa imepangwa, wabunge wapya sasa hivi wangekuwa wanamchagua Rais mpya.

Lakini kufanyika kwa zoezi hilo hadi siku ya mwisho iliyokuwa imewekwa haikuweza kufikiwa kwasababu wanasiasa walikuwa wanalUmbana.

Jaribio lolote la kueongeza muda wa utawala wa Farmajo litapingwa vikali – kwasababu wakosoaji wake wanasema amekuwa akijaribu kuchelewesha mchakato wa uchaguzi akitaka kujihakikishia muda zaidi wa kuhudumu.

Sasa hivi jumuiya ya kimataifa ndio itakayokuwa inasubiriwa - nchi za Marekani na Ulaya ambazo zilikuwa zikisaidia nchi hiyo katika masuala ya kiusalama na kifedha.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad