Watu 32 Wafariki Baada ya Ajali Mbaya za Magari



WATU 32 wamepoteza maisha na wengine watano kujeruhiwa vibaya, baada ya ajali mbaya kutokea usiku wa kuamkia leo ikihusisha magari matano likiwemo lililobeba jeneza, katika eneo la Kasese, Magharibi mwa Uganda.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu, Irene Nakasita, ajali hiyo imetokea baada ya gari lililokuwa limebeba jeneza liligongana na gari dogo namuda mfupi baadaye, gari jingine lililokuwa limewabeba waombolezaji, lilipoteza mwelekeo na kuyagonga magari yaliyogongana.

Muda mfupi baadaye, malori mawili yaliyokuwa yamebeba saruji, nayo yalipoteza mwelekeo na kuyagonga magari yaliyokuwa yamepata ajali, na kusababisha maafa makubwa.

Majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Kilembe katika wilaya ya Kisese huku baadhi miongoni mwao wakiwa na hali mbaya.




Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad