20 Wafariki Wa Corona Kenya, Idadi ya Vifo Yafikia 2,244

 


Watu 20 zaidi wamefariki ndani ya saa 24 kutokana na kupata Virusi vya Corona na kufanya idadi ya watu waliofariki kwa Corona nchini #Kenya kufikia 2,244


Aidha watu 460 wameripotiwa kuthibitika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo katika saa 24 zilizopita idadi inayofanya walioambukizwa kufikia 139,448


Wizara ya Afya imetangaza watu 178 kuwa wamepona 79 kati yao wakiwa ni wale waliokuwa wakijitibia nyumbani na hivyo idadi ya watu waliopona imefikia 94,361


Watu 1,590 wapo chini ya uangilizi wa kitabibu katika vituo vya afya na wengine 5,998 wanatibiwa majumbani mwao wakiwa wamejitenga, 200 wanapatiwa matibabu wakiwa katika hali mbaya na wamewekewa Oksijeni

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad