Chama Cha Upinzani Afrika Kusini Chakemea Kutumwa kwa Jeshi Kupambana na Waandamanaji




Chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) kimelaani kupelekwa kwa wanajeshi katika majimbo yaliyokumbwa na ghasia ya Gauteng na KwaZulu-Natal.
Katika taarifa iliyotolewa muda mfupi baada ya hotuba Rais Cyril Ramaphosa kwa taifa , EFF ilitoa wito wa "kutumiwa kwa suluhisho la kisiasa katika ghasia zilizoenea".

Chama hicho kilisema kupelekwa kwa wanajeshi mitaani sio suluhisho la machafuko ya wenyewe kwa wenyewe na kwamba haitakuwa sehemu ya uamuzi wowote wa kuhalalisha kupelekwa kwa jeshi.

EFF imesema mawakili wake wataandika barua kwa rais kujua "msingi wa kisheria wa kupelekwa kwa wanajeshi". Iliongeza kuwa itachukua "hatua zinazofaa" ikiwa rais atashindwa kujibu barua hiyo kwa masaa 12.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad