Hoteli yaporomoka China, Watu Wanane Wamepoteza Maisha





Watu wanane wameuawa wakati jengo la hoteli lilipoporomoka huko Suzhou, mkoa wa Jiangsu nchini China.

Jitihada za uokoaji zinaendelea kwa wale waliokwama chini ya kifusi.

Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Usimamizi wa Dharura, ilitaarifiwa kuwa timu za utaftaji na uokoaji zilitumwa kwa mkoa huo na maiti za watu 8 zimepatikana hadi sasa.

Katika taarifa hiyo, imebainika kuwa watu 14 waliokolewa kutoka kwenye kifusi cha hoteli na watu 9 hawakupatikana.

Imeelezwa kuwa hoteli hiyo iliyo na vyumba 54 ilifunguliwa 2018.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad