Undani wa Historia ya Msemaji wa klabu ya Yanga Haji Manara unatueleza mengu kuhusu Maisha yake na namna ambavyo angeweza kuja kuwa mwanasoka Hodari kabisa .
.
Haji Manara mbali na yeye kusomea Maswala ya mawasiliano kwa Umma amefanya kazi katika makampuni tofauti na hata kwenye nyanja ya kisiasa pia kabla ya kujiuzulu nafasi aliyokuwa nayo .
.
Historia yake inatuambia kuwa Alionyesha uwezo mkubwa wa kucheza mpira wa miguu akiwa mdogo na baada ya kuonyesha uwezo mkubwa Baba yake ambaye tayari naye pia amepita katika Njia hizo kwa mujibu wa Haji anasema Baba yake ilimbidi ambadilishie njia kwa kumpeleka Boarding School Mbeya huko Kijijini .
.
Kwenda mbeya mbali na kwamba ilikuwa ni mbali ilimfundisha namna ya kuishi na watu na wengine wanavyoishi, Alivyorudi kutoka Mbeya aliendelea na kipaji chake akacheza timu mbali mbali ikiwemo Kariakoo united baadae Mafia mob united .
.
@hajismanara anasema alikuwa sio anakiwango hicho kama cha mzee wake ila kama angepewa fursa angekuwa hatari zaidi lakini Baba yake aliona hana future na mpira labda kwa sababu changamoto ambazo yeye aliziona kipindi tofauti na sasahivi kidogo wachezaji wananufaika .