Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeifuta kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleao (Chadema) Tanzania Bara, Tundu Lissu na wenzake wanne.
Ni baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.