Bifu la Alikiba na Diamond Platnumz Kwa Kiasi Kikubwa Sanaa Lina Changwia na Mashabiki..

 


Lakini hatuwezi kusema mashabiki hawa wana roho mbaya au wanakwamisha maendeleo ya msanii Fulani, hapana ilo nakataa!!

Kokote duniani ,kila nchi haya mambo yapo Wasanii kuwa na Bifu ni kitu cha kawaida sanaa ,Kwa sababu zao binafs , eitha zenye manufaa au zenye hasara!!

Kwa ishu ya alikiba na Diamond , mashabiki wameikuza hii bifu vibaya mnoo,,upande mmoja wa ushbikii Unadai mmoja anajua kuimba kuliko mwingine, . Hii ishu inazidi kuchocheaa Sana Bifu Lao!

Tukirudi tu kwenye ule ukwelii, yaani tukiweka ushabiki pembeni ukweli ni huu

"Kila msanii anajua kuimba kulingana na nafasi yake, na Aina ya nyimbo zake !! Na wote Wana umuhimu Sana katika jamii kulingana na mood ya msikilizaji"

Ukihitaji vibe ,kudance utamsikiliza ,simbaa🔥

Ukihitaji sauti nzuri ,na mambo ya hisia utamsikiliza alikiba

Kila msanii akiulizwa kuhusu Alikiba na diamond anatoa maoni kua wote wanajua kuimba!

Tunafahamu kua fally ipupa yupo Tanzania , amehojiwa tumeona amekiri wazi kuwa alikiba anajua kuimba sanaa na pia amezungumza kwamba,

Nyimbo Kali Kwa upande wake yeye ni nyimbo ya inama, ya diamond , hapa anamaanisha pia anamkubali Diamond , na anajua kuimba pia.

Kwahiyo tunapofanya ushabiki tusiunganishe na chuki , Kama unamshabikia alikiba usisite pia kumshabikia Simba!! Wote hawa ni ndugu zetu..

Kuhusu post ambazo tunakua tumemkandia msanii ,hizo wala zisiwaadae ,ni sehemu tu ya ushabiki na kuwafanya watu wa enjoy!!

Haya fikilia tusingekuepo watu kama Sisi stress zako za madeni na matatizo ungezipeleka wapi

Unapo comment Kwa kunitukana au Kwa kuchekaa ,unakua unapunguza stress ,kingine na comments zinakufanya uinjoy pia!!

Kwahiyo niseme tu nasisi ni watu wazuri tu ,na tuna umuhimu katika jamii ,so msichukulie mambo silias sanaa....

Sibongile.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad