Genge la majambazi wa Nigeria lakamatwa Afrika Kusini- ripoti




Vyombo vya sheria vya Afrika Kusini na Markani vimewakamata wanachama sita wa genge la majambazi wa Black Axe huko Cape Town, tovuti ya habari ya TimesLive inaripoti.


Kundi hilo , linaaminika kuhusika na mamia ya “Matapeli wa mapenzi”, liliripotiwa kukamatwa katika msako mapema Jumanne asubuhi.



Black Axe pia inadaiwa kulaghai makampuni mamilioni ya pesa kupitia uhalifu wa kimtandao ikihusisha biashara ya barua pepe za ulaghai.



Kundi hilo liliibuka miaka ya 1970 huko Nigeria ambapo lilifanya ubakaji, ukeketaji na mauaji ya kikatili. Wanachama wake waliendelea kujenga mtandao wenye nguvu wa kimataifa.



Lina uwepo mkubwa nchini Italia. Wanachama wake kadhaa walikamatwa nchini humo mwezi Aprili na kufunguliwa mashtaka karibu 100 ikiwa ni pamoja na biashara ya dawa za kulevya na ulanguzi wa watu, ukahaba na ulaghai wa mtandao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad