Juisi za Apple yaondolewa Sokoni Katika Mataifa Saba ya Afrika




Juisi ya Apple (tufaha) inayotengenezwa na kampuni ya Afrika Kusini ya Ceres imeondolewa sokoni katika mataifa saba ya Afrika kwa sababu ya kuwa na kiwango cha juu cha sumu ambayo inaweza kusababishia mtu kutapika na kupata kichefuchefu.
Juisi hizo zina aina ya sumu inayotolewa na baadhi ya kuvu{fungi} katika tufaha na bidhaa zake.

Uchunguzi wa maabara unaonesha kuwa juisi za Ceres zina kiwango kikubwa cha sumu zaidi ya kiwango kinachoruhusiwa kisheria 50 microgrammes kwa lita moja.

Juisi hizi zinauzwa Kenya, DRC, Zambia, Zimbabwe, Uganda, Seychelles na Mauritius.

Juisi hii ina soko kuu katika nchi za Mashariki na Kusini (Comesa) na wateja wametakiwa kurudisha juisi zilizonunuliwa tangu tarehe 14 na 30 Juni 2021

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad