Kwanini Kila Anayekuwa Karibu na Diamond Platnumz Naye Anakuwa Maarufu


Umewahi kujiuliza kwamba kwanini kila anayekuwa Karibu na @diamondplatnumz na yeye pia anakuwa maarufu au Star Kabisa. @diamondplatnumz anatoa wapi nguvu ya kufanya watu wake wa karibu kuwa mastaa?

Dancers, Wasanii wake, Maproducer, Wapiga picha, Wachumba, Watoto wake, Managers, Bodyguard na Familia yake yote ni famous. Hii nguvu anaitoa wapi? mbaya zaidi ukiwa nae mbali umaarufu unapungua kwa kasi sana.

Kuna pages nyingi za udaku Instagram zinashine kwa ajili ya kusupport au kuponda kazi za Diamond na familia yake. Mwijaku ameanza kufahamika vema baada ya kumdiss mond.
Shilawadu kimyaaaaaaaaaa coz hawakavi stories za mond na familia yake ambazo ndio zilikipaisha kipindi.

Millard ayo ni moja ya waathirika wakuu, covers na stories za mond zilikuwa zinampa pesa sana YouTube lakini kwa sasa haonyeshi kitu chochote cha mond.

Hakuna mtu yoyote nchini Tanzania mwenye Influence kama ya Diamond. Hoja yangu ya msingi huyu bwana nguvu hii anaipata wapi ya kufanya watu wake wa karibu kuwa maarufu sana?

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad