Mo Dewji "Napata Hasara Simba Napoteza Hela Nyingi Sana"


MFANYABIASHARA maarufu Tanzania na Afrika kwa ujumla ambaye pia ni mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji ‘Mo Dewji’ akihojiwa na Shirika la Utangazaji la CCN nchini Marekani amesema amewekeza kwenye klabu ya (10) kwa ubora Barani Afrika na ina mashabiki Tsh milioni 40.

Amesema pesa zake zinapotea kwani hapati faida, mpaka sasa ametumia zaidi ya dola za Kimarekani milioni 20 bila kupata faida, lakini amewekeza kutokana na mapenzi tu, lakini klabu hiyo haimuingizii faida yeyote.

“Simba SC ina miaka 85, ina mashabiki 40m, ndani ya miaka 4 nimewekeza dola milioni 20 ili iwe miongoni mwa klabu 10 bora Afrika. Tuna malengo makubwa. Hakuna biashara ila napoteza hela nyingi. Nafanya haya kwa mapenzi yangu sababu naipenda sana Simba,” amesema Mo Dewji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad