Ongezeko la Wanaume Kuomba Picha za Utupu Janga la Dunia..Je Wanazifanyia Nini?


Inawezekana umewahi kujiuliza, kwa nini boyfriend/girlfriend wangu anataka picha zangu za uchi/utupu? Hizo picha huwa anazifanyia kitu gani na zina faida gani katika kuboresha mahusiano yenu?

Je, wanaume wanapata nini wanapoomba na kutumiwa picha za utupu?
»USHINDI, wanaamini kuwa ni washindi, kwamba hadi msichana ameamua kuvua chupi na kutuma utupu wake, basi amezimika sana.

»SILAHA, hizi picha zinaweza kuwa silaha kwa mwanaume wakati mkifarakana, anaweza kukutishia lolote na mwanamke ukatii kwasababu tu anapicha zako za nyuchi.

»KUJIRIDHISHA, wengine hutumia utupu wa wapenzi wao kufanya masturbation.

Trend ya kutuma picha za utupu imeongezeka kwa kasi, hasa baada ya watu wengi kuweza kumiliki smartphones, watu hutuma picha zao za kifua, tak*, nakadharika, nakadharika.

Lakini tujue kuwa;
»Kutuma picha za utupu sio salama, hakuna "100% privacy" katika ulimwengu wa kidijitali. Kuna hackers wengi, siku hizi teknolojia inapanuka kila siku, kuna kuachana na kulipiana visasi, tuwe makini.

Wanaume ni wajanja, anasema tu "nikimaliza kuangalia nitazifuta", wanawake msidanganywe, huwa hazifutwi. Tusiwe malimbukeni wa teknolojia, tutumie teknolojia kwa faida.

Je, umewahi kutuma/kutumiwa picha za utupu? Unajisikiaje leo ukikumbuka zile picha zako ulizomtumia ex gf/bf? Naamini katika hili wengi wetu ni wahanga wa hili jambo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad